• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Usafi na Mazingira
    • Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria
      • Sheria ndogo za mazingira
      • Sheria ndogo za Halmashauri
      • Tozo za Leseni za Biashara
    • Fomu
    • Miongozo
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari

Hospitali ya Mji wa Kahama yatoa Vipimo bure kwa wazee Kuelekea "Nyerere Day"

Imewekwa: October 13th, 2018

Uongozi wa Hospitali ya Mji wa Kahama na Ofisi ya Ustawi wa Jamii inamuenzi Baba wa Taifa kwa kutoa huduma ya vipimo bure kwa wazee. Huduma hii ni ya siku mbili kuanzia leo na kumalizika kesho Oktoba 14. Akifungua huduma hiyo Mgeni Rasmi Ndg. Timothy Ndanya Katibu Tawala wa Wilaya ya Kahama ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kahama ameimwagia sifa Halmashauri ya Mji wa Kahama kwa kuweza kuienzi hii siku kwa kuonesha upendo kwa Wazee. Aidha amewahakikishia Wazee waliojitokeza kupima afya zao kuwa Serikali inaendelea kuwaboreshea huduma za afya kwani Wazee ni tunu.

"Niwaombe watumishi wa afya kufanya kazi kwa Weledi, na niwaombe wazee wangu ikitokea umepewa lugha ya kejeli au kunyanyaswa na mtoa huduma wa afya Ofisi yangu ipo wazi, tuwasiliane ili tuweze kuchukua hatua stahiki". Amesema Ndanya.

Katika  hatua nyingine Bw. Ndanya amewaomba wazee kuwa walimu kwenye Malezi ya Vijana na ameahidi kusimamia Sera ya wazee itekelezwe.

Awali akiongea katika utangulizi Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Halmashauri ya Mji wa Kahama Ndg. Wilfred Biragu ameiomba Serikali kutekeleza yale yaliyoahidiwa kwenye Maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika Tarehe 1 Oktoba 2018.

Kwa upande wake Katibu wa Baraza la wazee Mji wa Kahama Ndg. Anderson Lyimo ameishukuru Halmashauri ya Mji wa Kahama kwa kuweza kuwajali kwa kuwapa nafasi ya kupima afya zao ambapo itawasiadia kujua hali walizo nazo na namna ya kujiweka sawa.

Afisa Ustawi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Ndg. Abraham Kibakaya amesema kuwa wanaendelea kuwahudumia wazee kwa namna ya kipekee na tayari katika ofisi yake kuna dawati la kusikiliza kero za wazee. Amesema kuwa kwa Halmashauri ya Mji wa Kahama jumla ya wazee 6,347 wamepewa Kadi za Bima ya Afya .




Matangazo

  • INGIA HAPA KUPATA SALARY SLIP YAKO January 01, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    May 14, 2025
  • Kanuni za Maadili za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025

    April 19, 2025
  • Uboreshaji Awamu ya Pili wa Daftari la Mpiga Kura kuanza Mei Mosi

    April 16, 2025
  • Naibu Meya Manispaa ya Kahama ahimiza Ulipaji wa Ankara za Hati

    April 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Ufafanuzi wa Mikopo ya Asilimia Kumi Manispaa ya Kahama
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Picha Mbalimbali
  • Matukio Mbalimbali
  • Kupata Salary slip
  • Mapato na Matumizi Oktoba -Desemba 2017
  • Taarifa ya Miradi ya Mwaka 2016/2017
  • Zabuni mbalimbali
  • Taarifa kwa umma

Viunganishi vinavyohusiana

  • MFUMO WA KUWASILISHA MALALAMIKO
  • Ajira Serikalini
  • NECTA
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Tovuti ya Ikulu

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Barabara ya Boma, Kahama

    Anuani ya Posta: P.O.Box 472

    Simu: +255 282710032

    Simu: +255719679464

    Barua pepe: md@kahamamc.go.tz / info@kahamamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017. Halmashauri ya Manispaa Kahama. Haki zote zimehifadhiwa